•Ulcers ama vidonda vya tumbo ni michubuko ama vidonda vinavyotokea kwenye njia ya mfumo wa chakula hasa mfuko wa tumbo (stomach)na sehemu ya awali ya utumbo mwembamba (duodenum).
Ni nini husababisha ulcers?
•Kwa kawaida mwili hutengeneza asidi na homoni mbalimbali kwa ajili ya kusaidia mmeng’enyo wa chakula kwenye mfuko wa chakula k.m HCL na Gastric juice. Vimelea hivi vikizidi husababisha michubuko au kudhoofisha kuta za ndani ya tumbo na hivyo kuongeza hatari ya mtu kupata vidonda vya tumbo.
****Maambukizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori husababisha mtu aliye kwenye hali hiyo kupata vidonda vya tumbo.****
•Mwili hujikinga dhidi ya asidi ya tumboni kwa:
–Kuruhusu chakula kisafiri kwa spidi inayostahili –Kutengeneza alkali ili kuleta uwiano na asidi iliyotengenezwa tumboni hivyo chakula kilicho katika utumbo mwembamba huwa hakina asidi wla alkali.
Vitu hatarishi vinavyoweza kupelekea vidonda vya tumbo ni nini?
•Msongo wa mawazo (stress)
•Vinywaji vyenye caffein kama kahawa
•Sigara(nicotine)
•Pombe
•Kutokuwa na uwiano sahihi wa kula chakula k.m kula kupitakiasi usiku kwa sababu mchana ulishinda njaa.
•Magonjwa k.m ini
•Kutumia dawa hasa za NSAIDs k.k aspirin
Dalili za vidonda vya tumbo
•Mara
nyingi hutokana na eneo kilipo kidonda
Mfuko wa tumbo(gastric)
- maumivu makali ya tumbo saa1-2 mara baada ya kula
Mwanzo wa utumbo mwembamba (duodenum)
-maumivu makali ya tumbo kabla ya kula (hupungua pale unapokula au maziwa)
-maumivu makali ya tumbo usiku wa manane
Dalili za jumla
-kupungukiwa na damu mwilini
-choo kuwa na rangi nyeusi(melena)
-kutapika damu (haematemesis)
-kukosa hamu ya kula
-kuwa na kiungulia
-maumivu ya kifua
Dalili za hospitali
-kuuma tumbo akiguswa
-tumbo kuunguruma (succission splash)
- H pylori wakiotesha damu
Madhara ya vidonda vya tumbo
•Kwa watoto ni utapiamlo
•Kutoboka kwa utumbo
•Maambukizi ya bakteria wengine kupitia katika kidonda
•Kupungukiwa damu
•Kupungukiwa uzito
•Vidonda kupeleka magonjwa mengine kama gastric outlet
obstruction(GOO)
Matibabu
•Matibababu ya madawa ya hospitali
mgonjwa hupewa dawa hospitali za kupunguza asidi na kuua bacteria wa H pylori. Kidonda hubaki kwa muda mrefu k.m omeprazole, flagyl na amoxicilin kwa walau wiki mbili.
•Matibabu ya upasuaji hospitali
–Hii ni kwa baadhi ya wagonjwa ambao vidonda vyao ni sugu, vikubwa vyenye hatari ya kutoboa
utumbo
–Hii ni kwa baadhi ya wagonjwa ambao vidonda vyao ni sugu, vikubwa vyenye hatari ya kutoboa
utumbo
Matibabu asilia ya vidonda vya tumbo
•Matibabu asilia ya vidonda vya tumbo inahusisha virutubisho mbalimbali muhimu kwa ajili ya kuleta uwiano wa asidi mwilini, kuua bakteria wa H pylori na kuponya vidonda vyenyewe pamoja na mabadiliko kwa mtazamo wa maisha bora zaidi.
Mgonjwa wa vidonda vya tumbo afanye yafuatayo:
•Kunywa maji safi na salama lita 2-3
•Kupunguza matumizi ya kahawa yenye caffeine
•Kuepuka kula mlo mmoja mwingi baada ya kukosa mingine k.m usiku
•Epuka vyakula vinavyokuletea aleji
•Asinywe pombe
•Kutotumia dawa kama za NSAIDs kama aspirini
•Asivute sigara
•Ale
chakula kwa wastani kwa vipindi
•Asitumie dawa za NSAIDs kama aspirini
•Atumie virutubisho muhimu vya asilia kwa ajili ya ugonjwa
wake wa vidonda vya tumbo
Virutubisho muhimu kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo
•Mgonjwa wa vidonda vya tumbo anakabiliwa na:
- maambukizi ya bakteria wa H pylori
- kuta dhaifu za tumbo
- vidonda katika tumbo
- upungufu wa damu
PATA VIRUTUBISHO MUHIMU KWA AJILI YA TATIZO HILO
PHONE: =+255717962720
= +255767962720
0 comments:
Post a Comment